ASACOHUB
ASACOHUB
ASACHIFU COLLEGES HUB, Loading....
📞 +255 679 852 485  |  ✉ info@asacohub.ac.tz
About Contact Help
How It Works

Jinsi ASACOHUB Inavyofanya Kazi

Hatua rahisi kwa wanafunzi na vyuo kuanza kutumia jukwaa letu. Kila kitu kimeundwa kuwa rahisi, haraka, na salama.

1+ Colleges
2+ Programs
1+ Students
1+ Applications

Chagua Upande Wako

Kila upande una hatua 6 rahisi za kufuata.

01

Jisajili Bure

Fungua akaunti bure kwa jina lako, barua pepe, na namba ya simu. Thibitisha kwa OTP inayotumwa kwenye simu yako.

Inachukua dakika 2 tu
02

Kamilisha Wasifu

Jaza taarifa zako za kielimu (Form IV, Form VI), region, na documents. Pakia certificate na profile photo.

Documents zina hakikiwa
03

Subiri Uthibitisho

SuperAdmin anahakiki taarifa zako. Ukipitishwa, unapata taarifa kwa SMS na Email na unaweza kuanza kuomba vyuo.

Kawaida ndani ya saa 24
04

Tafuta Chuo

Vinjari vyuo vilivyothibitishwa, chuja kwa Health/Non-Health, region, na ownership. Linganisha programs na fee.

Vyuo 50+ vilivyothibitishwa
05

Omba Vyuo (Hadi 3)

Chagua vyuo hadi vitatu unavyopenda na uwasilishe maombi yako. Chuo kinapokea maombi yako kama lead.

Hakuna malipo kwa mwanafunzi
06

Pata Joining Instructions

Ukiidhinishwa na chuo, lipia application fee, pakia proof, na upate joining instructions kwenye akaunti yako.

Moja kwa moja kwenye akaunti
01

Jisajili Chuo

Fungua akaunti ya chuo kwa jina la mwakilishi. Weka barua pepe ya chuo na namba ya simu ya mawasiliano.

Dakika 3 tu
02

Wasilisha KYC

Pakia NACTVET RegNo, certificate halali, picha za chuo, programs, fee structure, na taarifa nyingine muhimu.

NACTVET inahitajika
03

Thibitishwa

ASACOHUB inahakiki na kuthibitisha chuo chako. Ukithibitishwa, chuo chako kinaonekana kwa umma na kupokea leads.

Kawaida ndani ya siku 2
04

Pokea Leads

Pokea maombi ya wanafunzi kama leads. Unaona taarifa za kielimu (bila contacts) ili kuamua kukubali au kukataa.

Notification kwa SMS + Email
05

Lipia Lead (TZS 2,000)

Kubali lead na ulipie TZS 2,000 kwa mobile money. Ukishalipia, taarifa kamili za mawasiliano zinafunguliwa.

M-Pesa, Tigo Pesa, Airtel, Halo
06

Karibisha Mwanafunzi

Wasiliana na mwanafunzi, fanya admission kwenye mfumo, na pakia joining instructions kwa mwanafunzi.

Jibu ndani ya siku 30

Kwa Nini Uchague ASACOHUB?

Sababu sita zinazotufanya tuwe jukwaa bora la kuunganisha wanafunzi na vyuo.

Vyuo Vilivyothibitishwa

Vyuo vyote kwenye ASACOHUB vinahakikiwa na kuthibitishwa. Hakuna vyuo vya uongo.

Urahisi wa Kuomba

Omba vyuo hadi vitatu kwa mchakato rahisi, bila usumbufu wa karatasi.

Taarifa kwa Wakati

Pokea taarifa za maombi yako kwa SMS na Email, wakati wowote.

Usalama wa Taarifa

Contacts zinaonekana kwa chuo tu baada ya kulipia lead. Faragha yako inalindwa.

Ranking ya Vyuo

Vyuo vinapangwa kwa utendaji, siyo idadi ya leads pekee. Hii inakuza ubora.

Msaada wa Muda Wote

Timu yetu ipo kukusaidia wakati wote, kwa simu, barua pepe, au WhatsApp.

Maswali ya Haraka

Majibu ya maswali yanayoulizwa mara kwa mara.

Je, kutumia ASACOHUB ni bure kwa wanafunzi?

Ndiyo, kwa wanafunzi kujiunga na kuomba vyuo ni bure kabisa. Vyuo ndio hulipia lead ili kupata taarifa zako za mawasiliano.

Ninaweza kuomba vyuo vingapi?

Unaweza kuomba vyuo hadi vitatu (3) kwa wakati mmoja. Ukishajibiwa, unaweza kuomba tena kama unataka.

Gharama ya lead kwa chuo ni kiasi gani?

Gharama ya lead ni TZS 2,000/= kwa mwanafunzi mmoja. Unalipia tu baada ya kukubali lead na kuona taarifa za kielimu.

Nini kinatokea kama chuo hakitajibu?

Kama chuo hakitajibu ndani ya siku 30, ASACOHUB inatoa warning. Kama bado, chuo kinaweza kubanwa na profile kuondolewa.

Una Swali?

Wasiliana nasi moja kwa moja na timu yetu itakusaidia haraka.

Uko Tayari Kuomba?

Fungua akaunti yako bure na anza kuomba vyuo hadi 3.