ASACOHUB
ASACOHUB
ASACHIFU COLLEGES HUB, Loading....
📞 +255 679 852 485  |  ✉ info@asacohub.ac.tz
About Contact Help
Legal

Sheria na Masharti

Tafadhali soma Sheria na Masharti haya kwa makini kabla ya kutumia jukwaa la ASACOHUB. Kwa kutumia huduma zetu, unakubali kufungwa na masharti haya.

Ilisasishwa: 13 Septemba 2026 Dakika 7 za kusoma 12 Sehemu
Muhimu: Kwa kutumia ASACOHUB, unakubali Sheria na Masharti haya. Kama haukubali, tafadhali usitumie huduma zetu.

1. Kukubali Masharti

Kwa kutumia jukwaa la ASACOHUB (linalopatikana kupitia tovuti yetu, simu, au njia nyingine yoyote), unakubali kufungwa na Sheria na Masharti haya. Kama haukubali masharti haya, tafadhali usitumie jukwaa letu.

Masharti haya yanatumika kwa wanafunzi, vyuo, wazazi, walezi, na watumiaji wengine wote wa ASACOHUB. Tunahifadhi haki ya kubadilisha masharti haya wakati wowote, na mabadiliko yataanza kutumika mara moja yanapowekwa kwenye tovuti yetu.

2. Maelezo ya Huduma

ASACOHUB ni jukwaa la kidijitali linalounganisha wanafunzi wanaotafuta vyuo na vyuo vinavyotafuta wanafunzi Tanzania. Huduma zetu ni pamoja na:

  • Kuonyesha orodha ya vyuo vilivyothibitishwa na NACTVET.
  • Kuwezesha wanafunzi kuomba vyuo hadi vitatu (3) kwa wakati mmoja.
  • Kuwezesha vyuo kupokea maombi kama leads na kulipia ili kupata taarifa za mawasiliano.
  • Kuwezesha mchakato wa application fee, admission, na joining instructions.
  • Kutoa ranking ya vyuo kwa kuzingatia utendaji.
  • Kutoa taarifa kwa SMS na Email kuhusu maombi na malipo.

ASACOHUB haitoi udhamini wa kukubaliwa kwenye chuo chochote. Uamuzi wa kukubali au kukataa mwanafunzi ni wa chuo husika.

3. Akaunti ya Mtumiaji

Ili kutumia huduma zetu, unahitajika kufungua akaunti. Unakubali:

  • Kutoa taarifa sahihi, kamili, na za sasa wakati wa kujisajili.
  • Kuhifadhi password yako kwa usiri mkubwa na kutokuishiriki na mtu mwingine.
  • Kuwajibika kwa shughuli zote zinazofanyika kwenye akaunti yako.
  • Kutujulisha mara moja kama unaona akaunti yako imevamiwa au kutumika vibaya.
  • Kutokuunda akaunti kwa kutumia taarifa za uongo au za mtu mwingine.

Tunahifadhi haki ya kufuta au kusimamisha akaunti yoyote inayokiuka masharti haya bila taarifa ya awali.

4. Wajibu wa Wanafunzi

Kama mwanafunzi anayetumia ASACOHUB, unakubali:

  • Kutoa taarifa sahihi za kielimu, ikiwemo Form IV Index, Form VI Index, na documents.
  • Kutuma maombi kwa vyuo ambavyo unakusudia kweli kujiunga.
  • Kulipia application fee kwa chuo ulichokubaliwa kwa wakati.
  • Kutuma proof ya malipo kwa usahihi (payslip + Transaction ID).
  • Kutokuomba vyuo zaidi ya vitatu (3) kwa wakati mmoja.
  • Kutokutumia mfumo kwa udanganyifu, ulaghai, au shughuli zisizo halali.
  • Kufuta akaunti yako kama huwezi kuendelea na mchakato.

ASACOHUB haiwajibiki kwa uamuzi wa chuo kukukataa au kukukubali. Pia haiwajibiki kwa ada za chuo (application fee, tuition, n.k.).

5. Wajibu wa Vyuo

Kama chuo kinachotumia ASACOHUB, mnakubali:

  • Kutoa taarifa sahihi za chuo, ikiwemo NACTVET RegNo na certificate halali.
  • Kutoa taarifa sahihi za programs, fee structure, na capacity.
  • Kujibu maombi ya wanafunzi ndani ya siku 30 (thelathini).
  • Kulipia lead (TZS 2,000) kwa wakati ili kupata taarifa za mawasiliano.
  • Kutokatumia taarifa za wanafunzi kwa madhumuni mengine zaidi ya admission.
  • Kutoa joining instructions kwa wanafunzi walioadmitiwa.
  • Kutokutumia mfumo kwa udanganyifu au shughuli zisizo halali.

Chuo kinachokiuka masharti haya kinaweza kupata warning, kubanwa, au kuondolewa kwenye jukwaa letu.

6. Malipo na Gharama

Malipo kwenye ASACOHUB yanafanyika kwa njia ya mobile money kupitia SplashPay. Unakubali:

  • Kulipia gharama ya lead (TZS 2,000) kwa kila mwanafunzi unayetaka kupata taarifa zake.
  • Malipo ya lead hayarudishwi (no refund) kwa sababu lead inafunguliwa mara moja.
  • Application fee inalipwa moja kwa moja kwa chuo, siyo ASACOHUB.
  • Kutoa taarifa sahihi za malipo na kuhifadhi risiti.
  • Kutokutumia njia za malipo zisizo halali.

ASACOHUB haiwajibiki kwa malipo yoyote yanayofanyika moja kwa moja kati ya mwanafunzi na chuo.

7. Usalama na Faragha

Tunalinda taarifa zako kwa kutumia teknolojia ya kisasa. Hata hivyo, unakubali:

  • Kutokuweka taarifa nyeti kwenye maeneo ya umma ya jukwaa letu.
  • Kutujulisha mara moja kama unaona taarifa zako zimevuja.
  • Kukubali kwamba hakuna mfumo wa mtandao ambao hauna hatari kabisa.
  • Kutokulaumu ASACOHUB kwa matukio yanayotokana na mazingira ya nje ya udhibiti wetu.

Taarifa zako za mawasiliano zinaonekana kwa chuo tu baada ya chuo kulipia lead. Hii inalinda faragha yako.

8. Haki Miliki

Maudhui yote kwenye ASACOHUB, ikiwemo lakini siyo tu: maandishi, graphics, logos, icons, picha, na software, ni mali ya ASACOHUB au watoa huduma wake, na yanalindwa na sheria za haki miliki za Tanzania.

Hauruhusiwi:

  • Kunakili, kusambaza, au kutumia maudhui yetu bila idhini ya maandishi.
  • Kutumia jina letu, logo, au trademark kwa njia yoyote bila idhini.
  • Kufanya reverse engineering ya mfumo wetu.

9. Kikomo cha Wajibu

ASACOHUB haiwajibiki kwa:

  • Uamuzi wa chuo kukukubali au kukukataa.
  • Ubora wa elimu au huduma zinazotolewa na chuo.
  • Malipo yoyote yanayofanyika kati ya mwanafunzi na chuo.
  • Hasara yoyote inayotokana na matumizi ya jukwaa letu.
  • Kukatika kwa huduma kwa sababu za kiufundi, mitandao, au nguvu za asili.

Jukwaa letu linatolewa "kama lilivyo" (as-is) bila dhamana yoyote ya aina yoyote.

10. Kufuta Akaunti

Unaweza kufuta akaunti yako wakati wowote. ASACOHUB inaweza pia kufuta au kusimamisha akaunti yako kama:

  • Unakiuka masharti haya.
  • Unatoa taarifa za uongo.
  • Unatumia mfumo kwa udanganyifu.
  • Unasababisha madhara kwa watumiaji wengine.

Baada ya kufuta akaunti, taarifa zako zinaweza kuhifadhiwa kwa muda kwa madhumuni ya kisheria na audit.

11. Mabadiliko ya Masharti

ASACOHUB ina haki ya kubadilisha masharti haya wakati wowote. Mabadiliko yataanza kutumika mara moja yanapowekwa kwenye tovuti yetu.

Ni wajibu wako kuangalia mara kwa mara kama kuna mabadiliko. Kuendelea kutumia jukwaa letu baada ya mabadiliko kunamaanisha unakubali masharti mapya.

12. Mawasiliano

Kama una swali lolote kuhusu Sheria na Masharti haya, tafadhali wasiliana nasi:

  • Barua Pepe: info@asacohub.ac.tz
  • Simu: +255 679 852 485
  • WhatsApp: +255 679 852 485
  • Ofisi: Arusha, Tanzania

Timu yetu itafurahi kukusaidia kwa maswali yoyote unayoweza kuwa nayo.

Uko Tayari Kuomba?

Fungua akaunti yako bure na anza kuomba vyuo hadi 3.